NAULIZA HIVI NAULI ZA MIKOANI ZINAPANDA KIHOLELA?

Hili ni swali ambalo nilokuwa najiuliza kila wakati kwa maana nauli za magari ya mikoani hasa yanayokuja maeneo ya mikoa ya kusini zinapanda kiholela ukiazingatia na.huduma mbovu zinazotolewa na mabasi hayo. Hali hiyo nimeiona hivi karibuni baada ya kusafiri mara kadhaa kutoka dar es salaam kuja mikoa ya kusini mtwara na lindi. Kondakta anadiriki kukata bei ilioandikwa katika tiketi na kuandika ile anayoijua yeye. Kitendo ambacho kilisababisha malalamiko mengi toka kwa abiria. Je swala hili sumatra hamjaliona?

Ukizingatia lugha chafu za wafanya kazi wa basi hilo. Huu ni mfano mdogo tu wa basi la fresh coach linalofanya safari.zake mikoa ya kusini,sumatra mlitazame hili.
Share: