Makala Maalum-UJIO WA OBAMA TANZANIA NI KUFURU


Ulinzi mkali ambao tayari upo na utazidi kuonekana wakati wa Ujio wa Rais wa Marekani umewafanya baadhi ya Watanzania kujihisi wanadunishwa au kuabishwa. Wapo wengine ambao wanaona kuwa hatua mbalimbali za kiusalama zinazochukuliwa kumlinda Obama, Familia yake na ujumbe wake zinaonesha dharau na kutoaminiwa kwa vyombo vyetu vya ulinzi. Wengine wanafika mahali pa kuhisi kuwa Wamarekani wanatudharau sana kiasi kwamba wanatuchagulia nani aonene na Obama (rejea taarifa kwenye gazeti la Mwananchi la leo). Watanzania hawapaswi kujisikia hivyo hata kidogo.

Ulinzi wa Obama ni Mkali iwe ndani ya Marekani au Nje

Wakati wowote Rais wa Marekani anaposafiri iwe ndani ya Marekani au nje ya Marekani ulinzi wake ni mkali na karibu kamili (almost absolute). Kuanzia angalia ambalo anakuwepo (linakuwa no fly zone) na kuwa anaenda na kila kitu kinachoweza kutumika wakati wowote wa dharura yoyote inayoweza kufikirika kutokea. Kuanzia majanga ya moto, maji, maandamano ya kisiasa au hata mapinduzi ya kijeshi ulinzi wa Rais wa Marekani umejiandaa.

Mfano mzuri ni kuwa ikulu ya Rais pale DC – Jumba Jeupe – juu kabisa kuna mzinga wa kutungua ndege – surface to air battery. Lakini kubwa zaidi ni kuwa anga lote linalozunguka Ikulu hiyo ni eneo ambalo ndege haziruhusiwi kuruka (prohibited airspace). Na wakati wowote Rais anaposafiri mahali popote ndege haziruhusiwi kuruka juu yake. Anapotua kwenye uwanja kwa mfano hapa Detroit, hakuna ndege nyingine itakuwa inatua wakati huo huo! Sasa kama hili linatokea Marekani kwa kiasi gani linaweza kutokea Tanzania?

Ripoti hii maalum basi ina lengo la kuwasaidia Watanzania kutokwazika na kiasi cha ulinzi ambao Obama anakuja nao pamoja na usumbufu unaotokana na hilo. Kama msafara wa Rais Kikwete huwa unazusha usumbufu kwa watu basi wa Obama utasababisha kadhia – chukua msafara wa Kikwete zidisha mara 1000!

Mambo ya Kawaida ya Ulinzi wa Rais

Kwa yeye kuwa Rais wa Marekani Obama anapatiwa ulinzi wa hali ya juu kabisa labda wa kiongozi mwingine yeyote duniani. Anapokuwa ndani ya Marekani anapata bado ulinzi wa hali ya juu lakini pia ni kama mara ishirini hivi chini ya ulinzi anaopata akiwa nje ya Marekani. Hii ni kwa sababu moja kubwa anapokuwa Marekani anakuwa katika ulinzi wa vyombo vingi sana vya nyumbani na mahali popote anapokwenda. Hivyo, vitu kama magari watu, n.k vingi vinakuwa ‘mobilized’ kutoka ndani.

Ulinzi huu wa kawaida ni ule ambao mara nyingi watu wanaona (maafisa wa Usalama wanaoambatana na Obama popote anapokwenda) na ule ambao uko kwenye kivuli (usionekana) ambao unahusisha wataalamu wa mambo ya mawasiliano, wapelelezi, majasusi n.k

Rais wa Marekani anapotoka nje ya nchi anaenda pamoja na kikosi cha maaskari wasiopungua 500 hivi! Ulinzi wa Rais wetu huwa ni kama watu 40 hivi maafisa wa usalama na anapoenda nje namba hiyo inapungua kidogo. Tunaposema anakuja na watu 500 hivi kwa ajili ya ulinzi hawa ni nje ya wale wanaotangulia na wale ambao taifa husika linatoa. Kati ya hao walinzi kama 200 hivi ni makomandoo watupu wa jeshi la Marekani na Taasisi za kijasusi.


Rais Obama anaposafiri anasafiri na madaktari bingwa wasiopungua sita hivi pamoja na wapishi wake pamoja na choo chake! Pamoja na hao anaambatana na manesi na wataalamu mbalimbali wa afya ambao wanaweza kuingia kazini wakati wowote. Anapokuwa Washington DC hospitali moja iko maalum kwa ajili ya dharura ya Rais tu na ina mlango wake ambapo likitokea jambo basi Rais hatopata shida ya kuzungushwa! Pamoja na hivyo kuna kiasi cha lita za damu aina AB (damu ya Obama) ambayo pia inasafiri naye mahali popote kwa ajili ya dharura yoyote itakayohitaji kuwekewa damu. Hii ni ndani au nje ya Marekani
.
Ndege ya Obama ni chombo cha ulinzi wake pia


Ndege ya Rais wa Marekani maarufu kama Air Force One siyo ndege kama ndege nyingine. Ni ndege ambayo imetengenezwa kuhakikisha kuwa Rais anapokuwa angani anakuwa salama kabisa. Imeundwa kuweza kuhimili vishindo vya mlipuko wa Nyuklia katika umbali ambao inakuwa inaruka na mabawa yake hayapigiki risasi (armor plated). Ndege hiyo pia ina uwezo wa kuingilia mawasiliano ya rada ya nchi yeyote inaporuka (radar jamming) na pia inasafiri ikiwa na makanyaboya ya mizingi ya ardhini (earth to air missiles). Ndege hiyo ina namba za simu zisizopungua 85 ambazo zinatumika wakati wote kuhakikisha kuwa Rais anaweza kuwasiliana na mtu yeyote hata anapokuwa angani.
Obama katika ofisi yake angani
Anapokuwa ardhini helikopta za jeshi la Majini ambazo zinafuatana na rais nazo zinakuwa tayari kwa dharura yoyote. Rais wa Marekani ana helikopta 19 hivi ambazo zinaweza kutumiwa mahali popote. Hivyo, kwa mfano magari na helikopta zilizotumika Senegal si lazima zije Tanzania zinaweza kurudishwa Marekani wakati nyingine zikija Tanzania. Hili ni kweli pia kwa magari. KUtokana na ukaribu wa Afrika ya kusini na Tanzania bila ya shaka baadhi ya raslimali za ulinzi zilizotumika Afrika ya Kusini zitaletwa Tanzania vile vile.


Anasindikizwa na Meli za Kivita

Anapokuwa nje ya Marekani Rais wa Marekani anasindikizwa na meli za kivita zinazopokezana majukumu kwa kadiri anavyozunguka dunia na zinakuwa tayari wakati wote kuingilia kati ikibidi. Meli hizi zimejaa wanamaji na wapiganaji wa jeshi la majini (Marines). Wapiganaji wa meli hizi wako tayari wakati wowote kuingia kwenye nchi yoyote kumuokoa Rais wao endapo kuna tishio la maisha yake.

Gari lake nalo ni chombo cha ulinzi


Bila ya shaka katika ya vyombo vya ulinzi wa karibu kabisa kwa Rais ni gari lake analotumia ambalo limetengenezwa maalum kwa ajili ya kumpatia ulinzi wa hali ya juu. Hii ni pamoja na kuzuia risasi na milipuko ya mabomu ya mkono au rocket launcher! Na huwa hali moja bali kadhaa ili kuhakikisha watu hawajui Rais anakuwa katika gari gani hasa.



Rais anapokuwa ndani ya nchi nyingine

Rais wa Marekani anapokuwa ndani ya nchi nyingine suala la usalama linakuwa kwa kiasi kikubwa mikononi mwa nchi husika – kiufundi tu. Kimsingi hata hivyo ulinzi wake unahakikishiwa na Marekani na vyombo vyake vya ulinzi. Nchi husika na vyombo vyake vya ulinzi vinakuwa na mawasiliano ya mipango na hawa Wamarekani. Kutegemeana na nchi nan chi baadhi ya nchi zinaruhusiwa kwa kiasi kikubwa na nchi nyingine zinaona ni bora kuwaachia Wamarekani waendeshe ulinzi wenyewe – ili kukwepa lawama. Hivyo, Obama akienda Israeli kwa mfano walinzi wa Kiisraeli wanapewa nafasi kubwa kuliko kwa mfano akienda Afghanistan!



Lakini popote anapokwenda nchi husika inakuwa nyuma ya Wamarekani katika masuala ya ulinzi. Hili ni muhimu kulizingatia hasa kwa wale ambao wanaweza kudhani kuwa kwa kusisitiza kuwa Wamarekani wasimamie ulinzi wa Obama akiwa Tanzania basi Wamarekani wametudharau. Hili si kweli. Wamarekani wanatoa ulinzi huu wakishirikiana na watu wetu lakini kutokana na uzito wa ujumbe wenyewe na hasa hali ya usalama katika eneo letu (ikumbukwe tayari kulishatokea milipuko dhidi ya Wamarekani na wapo wenye kuvionea huruma vikundi vya kighaidi) ni wazi kuwa Wamarekani watakuwa na sharti la kusimamia ulinzi wote wao wenyewe na hilo sisi wengine tushukuru tu na labda kujifunza.


Japo wengi watauona ule ulinzi ulioko kwenye msafara ambao kwa kweli ni kidogo tu – ulinzi wenyewe ni ule ambao uko nje ya msafara; watakuwa kwenye mapaa, kwenye mahoteli, kwenye barabara na wengine watakuwa katikati ya watu wamechanganyika. Fikiria kwa mfano alipoenda India kiasi cha ulinzi kilikuwa karibu maafisa 10,000 wakitengeneza kama ngazi tano za ulinzi – na ninaamini hili litatokea Tanzania pia. Kulikuwa na watu karibu 1000 kwenye ziara ya India ambao walikuwa wanamlinda Obama ambao ni Wamarekani watupu!


Baadhi ya maafisa wanaomlinda Obama wanavaa miwani zenye camera ambazo zinarekodi na kurusha moja kwa moja sura na watu mbalimbali anaokutana nao au wanaojitokeza kumpokea. Yote ni katika kuhakikisha usalama

Kwenye njia zote ambao Obama na mke wake watakuwepo kutakuwepo na walenga shabaha (snipers) na majasusi wakitoa ulinzi. Kama Obama atalala Ikulu basi kutakuwa na maofisa wa Kimarekani wasiopungua 2000 hivi kuongeza ulinzi wa Ikulu yetu na kufanya Ikulu hiyo kuwa jengo salama zaidi duniani kwa usiku huo! Hili litakuwa pia kweli kama atalala kwenye mojawapo ya mahoteli yetu makubwa Jijini Dar. Kwenye nchi nyingine ambazo Rais hawezi kulala kwenye nchi husika basi meli ya kijeshi ya Kimarekani iliyoko karibu inageuzwa kuwa hoteli na wakati mwingine atalala angani wakati anarejea kwao!

Njia zote zina mbadala wake

Njia zote ambazo Obama atapitia tayari zitakuwa na mbadala waka (alternative routes) kiasi kwamba jambo moja likitokea kwenye njia moja tayari wanajua ni njia gani nyingine wachukue. Ni kwa sababu hiyo labda watu wa Dar-es-Salaam wameshauriwa kuangalia kama wanasababu ya kwenda mjini. Usumbufu wa aina hiyo hautatokea Dar tu na watu wakakwazika hata anapokuwa hapa usumbufu huo wengine tunaupata.

Mara mbili nimewahi kujikuta katikati ya mahali ambapo Rais anasafiri au kuja. Mara ya kwanza ilikuwa mara baada ya tukio la Septamba 11 wiki chache baadaye Rais Bush alikuja Detroit na alikuwa na mkutano hoteli moja iliyokuwa upande wa pili wa hoteli ambayo nilikuwa nafanyia kazi. Wakati huo nikifanya kazi kwenye mambo ya corporate reservations. Wiki kadhaa nyuma maajenti wa SS walikuja na kubook sakafu nzima ambayo haturukuhusiwa kumweka mtu yeyote! 

Mara ya pili mwaka jana wakati wa kampeni katika misafara yangu nikajikuta nabadilishiwa njia mahali ambapo palikuwa pamejaa mapolisi na barabara imefungwa – kisa Obama alikuwa na chakula cha jioni nyumbani kwa mtu mmoja wa wafadhili wake!

Hivyo, Watanzania wanapopata ugeni huu wasikwazike sana kama mawasiliano yao yataingiliwa – hasa wanaoishi Dar kwa sababu ya kuhakikisha kuwa hakuna bomu linaloweza kulipuliwa kwa simu – na hata kupata usumbufu mkubwa. Obama anakuja akiwakilisha taifa lenye nguvu kubwa zaidi duniani; nguvu hii kwa kiasi tu Watanzania wataiona na itawasumbua. Kwa wale wanaofikiria labda Obama ni kama Rais wa China wafikirie tena; ulinzi wa Obama ni mara nyingi zaidi ya ulinzi wa Xi Jinping.

Kwa hiyo kama ulishaanza kukwazika na kuona umedharauliwa hauna sababu tena; shangaa, furahia, jifunze na ombea aje na kuondoka salama yeye na msafara wake wote. Wakishaondoka, pumua kwa furaha.

Waandishi wa Tanzania na Watanzania wasiogope kuwapiga picha aafisa wa usalama wakiwa kazini. Hakikisha tu kwamba ukifanya hivyo huwawekei kizuizi wakiwa kazini.

Na. M. M. Mwanakijiji
Share:

OBAMA , ZUMA ANA KWA ANA

Rais wa Marekani Barack Obama, amesema uvumilivu na ujasiri wa Nelson Mandela ni mfano mwema kwa dunia na upendo wa dhati wa rais huyo wa zamani wa taifa la Afrika Kusini inaonyesha ni kwa namna gani alivyo na utu wa kibinadamu.
Bwana Obama ameongeza kuwa Mandela, alionyesha ukweli na ukakamavu ambao una maana kubwa katika utu wa kibinadamu ambao uliondoa tabaka la ubaguzi, udini na utaifa.
Rais huyo wa marekani ameyazungumza hayo mjini Pretoria baada ya mazungumzo na rais wa sasa wa Afrika kusini, Jacob Zuma.
Ziara hiyo ya bwana Obama ina lengo la kuongeza mauhusiano ya kibiashara lakini imetekwa na hisia za ugonjwa wa bwana Mandela ambaye amelazwa hospitalini kwa muda wiki tatu sasa kutokana na maradhi ya mapafu yanayosumbua mfumo wake wa kupumulia.
Katika kikao hicho wawili hao walizungumza na vyombo vya habari kuhusu ushirikiano wa mataifa yao kibiashara mbali na kutafuta suluhu ya kudumu katika mataifa yaliokumbwa na ghasia mashariki ya kati.
Ikulu ya White House imesema kuwa Obama pia atakutana na familia ya Mandela anayeugua maambukizi ya mapafu ili kuifariji.
Awali Rais Obama, aliye ziarani barani afrika alitoa shukran za dhati kwa uongozi ulioonyeshwa na Mandela.
Wakati wa ziara hiyo Obama pia atakutana na wanafunzi huko Soweto kabla ya kuelekea katika jela la Robben Island ambayo Mandela alihudumia kifungo chake cha miaka 27 wakati wa utawala wa ubaguzi wa rangi.


Share:

VIONGOZI WACHUJWA KUMPOKEA OBAMA

Wakati magari 150 ya msafara wa ziara ya Rais Barack Obama yamewasili nchini, majina ya mawaziri wa Tanzania yatakayoruhusiwa kumpokea kiongozi huyo kuchujwa na makachero wa FBI.

Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere, Moses Malaki aliliambia gazeti hili jana kuwa matayarisho ya ujio wa Rais huyo ni kabambe na hayajawahi kutokea katika historia ya Tanzania.

Pia alisema shughuli za kumpokea Rais Obama, anayetarajiwa kutua Jumatatu saa 8:40 mchana, zitaanza asubuhi kwa maofisa wa Marekani kushika majukumu yote katika uwanja huo, ikiwemo kuongoza ndege, ukaguzi wa abiria na mizigo, kwa maana wafanyakazi wa uwanja huo kuwa likizo kwa siku mbili.

“Wamesema kuwa wao watasimamia kila kitu kuanzia wageni watakaoingia na kutoka na wataamua nani aingie na kutoka,” alisema Malaki. Imebainika kuwa hata idadi ya maofisa wa Tanzania wakiwemo viongozi watakaompokea pia itapangwa na Wamarekani wenyewe.

“Wenyewe wana orodha yao na wanajua nani atakuwepo au hatakiwi kuwepo katika kundi la wageni watakaompokea Rais Obama,” alisema na kuongeza:

“Nilimuuliza Ofisa Usalama wa Marekani iwapo nitaweza kumwona Rais Obama, akaniambia: Utamwona ukibahatika kuwepo kwenye orodha.”

Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe naye alikiri kuwa mawaziri wanaotakiwa kuwepo katika msafara wa kumpokea Rais Obama ni wachache watakaochaguliwa tu na Wamarekani, baada ya kuyapitia na kuyachunguza majina hayo kwanza kabla ya kuyakubali.

“Hii sijawahi kuiona, hata sisi wenyewe tunateuliwa na wakishayapitia wataamua, nani aende au asiende,” alisema Chikawe.


Source Jamiiforum
Share:

MAOMBI ZAIDI KWA MANDELA NJE YA HOSPITALI ALIPOLAZWA

Mamia ya watu wanaendelea kukusanyika nje ya hospitali alikolazwa Nelson Mandela mjini Pretoria Afrika Kusini. Inaarifiwa Mandela bado yuko hali mahututi.
Wamekuwa wakimuimbia nyimbo na kumuombea nje ya hospitali. Wengine wamekusanyika katika iliyokuwa makaazi ya Mandela mtaani Soweto.

Afrika Kusini
Watu wana wasiwasi kuhusu hali y mandela lakini pia wanataka kuonyesha wanavyojivunia kiongozi wao ambaye wanamuona kama baba wa taifa lao.
Mandela , rais wa kwanza mweusi Afrika Kusini, anaugua maradhi ya Mapafu.
Mamia ya wananchi walikesha kwa maombi maombi nje ya makaazi ya zamani ya aliyekuwa rais wa taifa hilo Nelson mtaani Soweto.
Rais Jacob Zuma amesema kuwa afya ya shujaa huyo aliyepigana dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini humo inaendelea kuimarika.
Mandela aliye na umri wa miaka 94 amekuwa hospitalini akiuguwa ugonjwa wa maambukizi ya mapafu.
Awali mwanawe wa kike, Makaziwe alisema afya ya babake inaendelea kuwa njema.
Aidha Makaziwe amevikashifu vyombo vya habari kwa kukita kambi nje ya hospitali alikolazwa shujaa huyo akisema wanahabari wanapaswa kumheshimu babaake.
Rais Jacob Zuma alisema Alhamisi kuwa hali ya Mandela iliimarika lakini bado yuko hali mahututi.
"leo angalau yuko sawa kidogo kuliko nilivyomwacha jana usiku,'' alisema Rais Zuma baada ya kuongea na madakatari wanaomtibu Mandela.
Bwana Zuma alifutilia mbali safari yake ya Msumbiji ili kumtembelea Mandela hospitalini.
Wakati huohuo mwanawe Mandela Makaziwe alisema Mzee 'bado yupo' na kuwa anaweza kuhisi mtu akimgusa.



Share:

OBAMA KUTEMBELEA KISIWA ALICHOFUNGWA MANDELA MIAKA 27

Rais Obama atazuru kisiwa cha Robben Island alikofungiwa jela rais wa zamani Nelson Mandela kwa miaka 27.
Rais wa Marekani Barack Obama leo Ijumaa anaelekea Afrika Kusini ambapo miongoni mwa shughuli zake atazuru kisiwa cha Robben Island  alikofungwa jela rais wa zamani Nelson Mandela kwa miaka 27.
 
Rais Obama anakwenda nchini humo wakati bw. Mandela akiwa katika hali mbaya ya afya. Rais huyo wa zamani anatibiwa katika hospitali moja ya Pretoria.
 
Alihamis rais Obama alisema ziara yake katika eneo ambalo watumwa wa Afrika waliondoka barani humo kwenda Amerika kaskazini imempa hamasa mpya ya kulinda haki za binadamu. Bw. Obama alitembelea kisiwa cha Goree kwenye ufukwe wa Senegal Alhamis.
 
Wanahistoria wanasema maelfu ya Waafrika wanaume kwa wanawake wakiwa wamefungwa minyororo walishikiliwa huko na kupitia kile kilichoitwa mlango wa kutorudi tena kupanda meli ya watumwa wakielekea bahari ya Atlantic.
 
Rais Obama alisema ziara yake katika kisiwa hicho ilimpa hisia kali na nafasi ya kutathmini upya biashara ya utumwa katika karne ya 16 na 19


Share:

MASHIRIKA,WANAFUNZI WAPINGA ZIARA YA OBAMA AFRIKA KUSINI

Huku Rais Barack Obama wa Marekani akiwa amewasili nchini Senegal hii leo katika duru yake ya kwanza ya safari barani Afrika, safari yake hiyo inakabiliwa na upinzani mkubwa huko Afrika Kusini ambayo itakuwa nchi ya pili kuitembelea kabla ya kuelekea Tanzania.
Duru zinaarifu kuwa idadi kubwa ya mashirika ya wafanyakazi, wanafunzi wa vyuo vikuu, mawakili na watetezi wa haki za binaadamu wanapinga vikali safari ya Rais Obama nchini humo. Muungano wa Jumuiya za Wafanya Kazi Afrika Kusini COSATU umewataka wafanyakazi nchini humo kufanya maandamano ya kupinga safari hiyo. Katibu wa masuala ya kimataifa wa COSATU, Bongani Masuku amesema kuwa, siasa za Marekani zimejikita zaidi katika kuzalisha na kukithirisha silaha za nyuklia na kusambaza silaha ulimwenguni, jambo ambalo linavuruga amani, uadilifu, demokrasia na haki za binadamu.
Jumuiya ya Mawakili wa Kiislamu nchini Afrika Kusini imetaka Rais Barack Obama wa Marekani atiwe mbaroni kwa kutenda jinai za kivita. Jumuiya hiyo ya mawakili imetaka Obama afikishwe kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Jinai, (ICC) huko, The Hague, Uholanzi. Makundi ya kisiasa nchini Afrika Kusini yameitaja Marekani kuwa mporaji wa maliasili na utajiri wa nchi za Kiafrika.


Share:

AFYA YA MANDELA BADO UTATA-ZUMA AHAIRISHA ZIARA YAKE YA MSUMBIJI

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amefutilia mbali ziara yake ya kwenda Musumbiji baada ya kumtembelea hospitalini aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela. Rais Zuma amesema kuwa Bwana Mandela yuko katika hali mbali ya afya.
Msemaji wa Zuma Mac Maharaj amesema kuwa hali yake imedorora zaidi katika saa 48 zilizopita.

Afrika Kusini
Mandela ambaye, ni rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, amelazwa hospitalini tangu tarehe 8 mwezi Juni akiugua maradhi ya mapafu.
Madaktari wanasemekana kufanya kila wawezalo kuhakikisha kuwa Mandela anapona.
Vikundi vya watu wenye huzuni mkubwa kuhusu hali ya afya ya Mandela, walikusanyika nje ya hospitali alikolazwa, wakiwa na ujumbe wa ugua pole kwa Mandela
Wadadisi wanasema kuwa wananchi wa Afrika Kusini wanaonekana kuwa tayari kwa habari zozote sasa kuhusu hali ya Mandela.
"tutasikitika sana ikiwa tutapata habari za kifo chake, lakini pia tutakuwa tunasherehekea maisha yake. Amefanya mambo mengi zaidi kwa nchi yetu,'' alisema kijana John Ndlovu, mwenye umri wa miaka 25.
Zuma alitarajiwa kuhudhuria mkutano wa marais nchini Msumbiji, hii leo lakini akaamua kuakhirisha safari yake.
Taarifa kutoka kwa ofisi yake ilisema kuwa anaendelea kuwapongeza wananchi wa Afrika Kusini wanaoendelea kuiombea familia ya Madiba.
Uamuzi wa Rais Zuma kufutilia mbali ziara yake ambako alitarajiwa kuhudhuria mkutano wa kikanda kuhusu uekezaji anaonyesha wazi kuwa hali ya Mandela inaendelea kuzorota zaidi kulingana na mwandishi wa BBC mjini Johannesburg Mike Wooldridge.



Share:

Dunia ina mambo-MWANAMKE ATUMIA "PERIOD BLOOD"KUFANYIA ART WORK

Chilean artist Carina Úbeda has saved five years’ worth of her own menstrual blood... for the sake of art.

 "I can not wear pads because they trigger an allergic reaction," Úbeda explained to Soy Chile. Instead of tossing her sanitary cloths aside, she decided to save the soiled fabric until inspiration struck.

For her current exhibition at the Center of Culture and Health in Quillota, Chile, entitled "Cloths," the artist put 90 used sanitary rags on display, each embroidered with words like "destroyed" and "production." Each embroidered rag is placed in an embroidery hoop and hung up, surrounded by dangling rotten apples symbolizing ovulation.

While some were disgusted by Úbeda's choice of material, others saw poignancy in the medium. "Male blood is celebrated for being brave while ours is a shame," one visitor told the Daily Mail. "This won't change until we release our body as the first stage of political struggle."


Share:

TATOO ZA WASANII KADHAA WA BONGOMOVIES ZILIZOWEKWA HADHARANI

Baada ya waigizaji kadhaa wa bongo movies kuendelea kuzianika tattoo zao mbalimbali zilizopo kwenye miili yao,sasa ni zamu ya mwigizaji Anyefanya vizuri sana kwenye tasnia ya filamu nchini CHUCHU HANS KICHUNYA kuziweka zake hadharani baada ya jana kuweka picha kadhaa kwenye mtandao zikionesha tattoo hiyo iliyoko maeneo ya kiunoni kwa juu kidogo.

Huyu anakuwa msanii mwingine tena wa bongo movies kuweka wazi tattoo zake baada ya waigizaji waliozoeleka kwenye jamii kwa tattoo zao kama Wema sepetu, Irene Uwoya, Jacquiline Wolper na Mainda







Share:

Makala- SATELITE YA KWANZA KURUSHWA ANGANI(SPUTNIK)

Ilirushwa Mnamo mwaka 1957
 The Soviet space agency launched Sputnik 1 into orbit to become the first artificial satellite.
 This success is considered the beginning of the Cold War's Space Race between the Soviet Union and the United States.
 The football sized satellite broadcast a radio signal during its 98 minute orbit for 22 days until the batteries ran out.
 Sputnik 1 re-entered the atmosphere and was destroyed on January 4, 1958.



Share:

MANDELA BADO HALI TETE,MAOMBI ZAIDI YATOLEWA

Askofu mkuu wa kanisa la kianglikana mjini Cape Town, Afrika Kusini, Thabo Makgoba, amejitolea kufanya maombi kwa niaba ya rais mstaafu Nelson Mandela ambaye anaugua sana hospitalini.
Kasisi huyo anamuombea Mandela aweze kupata nafuu na amewataka wananchi kumshukuru kwa yote aliyowafanyia.
Jamaa za Nelson Mandela wamekutana nyumbani kwake huko Kunu, huku hali yake ya afya ikizidi kudorora hospitalini, Pretoria.
Afya ya Bwana Mandela ilikuwa mbaya zaidi Jumapili.
Maombi hayo yalitolewa baada ya Askofuu huyo kumtembelea Mandela hospitalini ambako kiongozi huiyo wa zamani amekuwa akilazwa kwa wiki mbili na nusu zilizopita baada ya kuugua mapafu.
Vyombo vya habari nchini humo vinasema kuwa wajukuu wa rais huyo wa zamani wa Afrika kusini wanakutana nyumbani kwake kijijini katika mkoa wa Eastern Cape province, ambako viongozi wa kitamaduni wamealikwa.
Halikopta ya jeshi kadhalika zilionekana zikipaa karibu nyumbani kwa mandela. Afisi ya Rais jacob Zuma ilitangaza jumapili kuwa hali ya mzee Mandela ya afya ilikuwa mbaya sana.

Share:

"PINDA AWAOMBE RADHI WANANCHI"KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU

Kituo cha sheria na haki za binadamu-LHRC kimemtaka waziri mkuu Mh. Mizengo Pinda,kuwaomba radhi Watanzania kupitia bunge, kufuatia kauli aliyoitoa hivi karibuni bungeni mjini Dodoma , akiviamuru vyombo vya ulinzi na usalama likiwemo jeshi la polisi kuwadhibiti wananchi kwa kuwapiga pale wanapo kaidi amri halali inayotolewa na jeshihilo
source ITV
Share:

VYUO 100 BORA "UDSM NAFASI YA 6"

Kwa mujibu wa World University Web Ranking hii hapa ndio list ya vyuo 100 Tanzania ikiwa nafasi ya 6 kupitia chuo cha Dar es salaam.South afrika ikiongoza kushika nafasi za juu katika list hiyo.

CHEKI HAPA


1 University of Cape Town- South Africa

2 University of South Africa -South Africa

3 University of Pretoria -South Africa

4 Universiteit Stellenbosch-South Africa

5 University of the Witwatersrand-South Africa

6 University of Dar es Salaam-Tanzania


7 Cairo University-Egypt

8 University of KwaZulu-Natal-South Africa

9 The American University in Cairo-Egypt

10 Makerere University     -Uganda

11 Rhodes University-South Africa

12 University of the Western Cape-South Africa

13 Mansoura University-Egypt

14 University of Johannesburg-South Africa

15 Université Cheikh Anta Diop                -Senegal

16 Assiut University-Egypt

17 University of Nairobi- Kenya

18 Zagazig University-Egypt

19 University of Botswana-Botswana

20 Universit̩ Mohammed V РAgdal-Morocco

21 University of Ghana -Ghana

22 Universiteit van die Vrystaat     -South Africa

23 University of Ibadan        -Nigeria

24 Addis Ababa University-Ethiopia

25 North-West University-South Africa

26 Alexandria University-Egypt

27 Nelson Mandela Metropolitan University-South Africa

28 University of Zambia-Zambia

29 Université des Sciences et de la Technologie Houari Boumediène-Algeria


30 The German University in Cairo-Egypt

31 Obafemi Awolowo University-Nigeria

32 Universidade Eduardo Mondlane-Mozambique

33 University of Mauritius-Mauritius

34 Ain Shams University-Egypt

35 University of Lagos-Nigeria

36 Tanta University-Egypt

37 Université de Ouagadougou                -Burkina Faso

38 Kwame Nkrumah University of Science and Technology-Ghana

39 Université de la Reunion-Reunion

40 Université Nationale du Rwanda-Rwanda

41 Helwan University-Egypt

42 Cape Peninsula University of Technology-South Africa

43 University of Zululand-South Africa

44 Strathmore University- Kenya

45 Université Cadi Ayyad-Morocco

46 Al Akhawayn University-Morocco

47 Université d'Alger-Algeria

48 Université Mentouri de Constantine               -Algeria



49 Université Badji Mokhtar de Annaba               -Algeria

50 Université d'Oran-Algeria

51 Universit̩ Hassan II РCasablanca-Morocco

52 University of Fort Hare-South Africa

53 Université Abdelmalek Essadi-Morocco

54 Ahmadu Bello University-Nigeria

55 Jaamacada Muqdisho-Somalia

56 Jomo Kenyatta University of Agriculture and Technology- Kenya

57 University of Swaziland-Swaziland

58 University of Ilorin-Nigeria

59 Sudan University of Science and Technology               -Sudan

60 Universit̩ Mohammed V РSouissi- Morocco

61  Kenyatta University- Kenya

62 University of Khartoum-Sudan

63 University of Namibia-Namibia

64 Université de Batna-Algeria

65 University of Malawi-Malawi

66 Benha University-Egypt

67 Universit̩ Hassan II РMohammedia-Morocco

68 Al-Azhar University-Egypt

69 Fayoum University-Egypt

70 Université de la Manouba-Tunisia

71 University of Benin-Nigeria

72 Minoufiya University-Egypt

73 Durban University of Technology-South Africa

74 Université de Tunis El Manar-Tunisia

75 Université de Carthage-Tunisia

76 Tshwane University of Technology-South Africa

77 United States International University- Kenya

78 Université Abou Bekr Belkaid Tlemcen-Algeria

79 Polytechnic of Namibia-Namibia

80 Egerton University- Kenya

81 Université de Gabès                -Tunisia

82 Université de Sousse-Tunisia

83 Université d'Antananarivo-Madagascar

84 Minia University-Egypt

85 Moi University- Kenya

86 Université de Nouakchott-Mauritania

87 Université Mouloud Maameri de Tizi Ouzou-Algeria

88 University of Venda-South Africa

89 Central University of Technology-South Africa

90  Université Ibn Tofail               -Morocco
91 University of Zimbabwe-Zimbabwe

92 Suez Canal University-Egypt

93 University of Cape Coast-Ghana

94 Misr International University               -Egypt

95 University of Jos-Nigeria

96 University of Maiduguri-Nigeria

97 University of Limpopo-South Africa

98 The Hubert Kairuki Memorial University-Tanzania

99 Jimma University-Ethiopia

100 Modern Sciences and Arts University-Egypt







Share:

TAMKO LA SERIKALI POLISI KUUWA RAIA

Dar es Salaam.
 Serikali imetoa tamko bungeni kuhusu mauaji ya raia mikononi mwa polisi ikieleza kuwa sheria ya kanuni ya adhabu inaruhusu kutumia nguvu za kadiri hata kiasi cha kusababisha madhara au kifo.

Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kunukuliwa bungeni akiwataka polisi kuwashughulikia kwa kuwapiga watu wote wanaokaidi kutii sheria.

“…Nasema wapigwe tu, maana tumechoka sasa,” alisema Pinda alipojibu maswali ya papo hapo Alhamisi iliyopita.

Akisoma tamko hilo bungeni jana, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima alisema kuwa kifungu cha 18(B) na 18(C) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu kinatoa uwezo kisheria wa kutumia nguvu za kadiri hata ikibidi kiasi cha kusababisha madhara au kifo katika mazingira ya kisheria.

Aliyataja mazingira hayo kuwa ni pamoja na kuokoa uhai wa mtu mwingine, kuzuia madhara makubwa ya mwili yasitokee kwake au kwa mtu mwingine na kumzuia mtu anayetenda tendo ovu la kubaka au kunajisi mtoto au kufanya vitendo kinyume na maumbile.

Pia kumzuia mtu anayevunja nyumba usiku au unyang’anyi wa kutumia silaha au kuchoma nyumba moto au kufanya kitendo chochote kinachohatarisha uhai wa mtu au mali.

Alieleza kuwa Kifungu cha 18 na 18(A) cha Sheria ya Adhabu Sura namba16 iliyofanyiwa mapitio mwaka 2002, kinampa haki mtu yeyote akiwemo askari kujilinda, kumlinda mtu mwingine, kulinda mali yake au mali ya mtu mwingine ikiwemo ya Serikali na taasisi zake, ambayo iko chini ya uangalizi wake kisheria.

Kauli hiyo ya Serikali kuhusu mauaji ya raia mikononi mwa polisi, ilitolewa ikiwa ni ufafanuzi wa jibu la swali la nyongeza lililoulizwa bungeni Mei 28,2013 na Rashir Ally Abdalah (Tumbe-CUF), ambapo Silima alisema mauaji yanayofanywa na askari polisi ni mauaji ya kisheria. Kutokana na kauli hiyo, Mbunge wa Wawi, Hamad Rashi Mohammed aliomba mwongozo wa spika kupata ufafanuzi wa kauli hiyo, na jana Silima kutoa kauli ya Serikali kujibu mwongozo huo.

“Ikumbukwe pia kuwa, kifungu cha 29 cha Sheria ya Jeshi la Polisi na Polisi wasaidizi Sura322, pamoja na Kanuni za Kudumu za Utendaji za Jeshi la Polisi Na274, vinampa haki ya kisheria askari polisi kubeba na kutumia silaha za moto ikiwamo bunduki na mabomu katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku..,”alisema Silima.

Alifafanua kwamba katika kutafsiri sheria, kanuni na taratibu mbalimbali ikiwamo alizozitaja, mahakama katika nyakati tofauti imetoa msimamo wa kisheria juu ya suala hilo.

Akitoa mfano alisema: “Mathalan katika kesi ya Seif Mohamed Senzagala dhidi ya Jamhuri ya mwaka 1994 kama ilivyonukuliwa na Tanzania Law Report ukurasa wa 122, ambapo mshitakiwa (mwomba rufaa) alimjeruhi kwa panga mlalamikaji ambaye alimfuata nyumbani kwake na kuanza kumshambulia.”

Alisema katika kesi hiyo,mahakama ya rufaa pamoja na kuridhia uamuzi wa mahakama ya awali wa kumtia hatiani kwa kutumia nguvu kupita kiasi, ilibainisha kuwa mshtakiwa hakustahili adhabu kwani alitenda kosa lile wakati akijihami dhidi ya mashambulizi toka kwa mlalamikaji

source mwananchi.
Share:

LOWASA KUGOMBEA URAISI 2015"MAONI YA WANAFUNZI UDOM"


Waziri Mkuu aliyejiuzuru na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Ngoyai Lowasa alipotembelewa na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha DODOMA (UDOM) ambao walitokea katika shule zasekondari za kata.

Wanafunzi hao, pamoja na kumpongeza Mh. Edward Lowassa kwa kuasisi na kusimamia ujenzi wa shule za sekondari katika ngazi ya kata pia wamemtaka achukue fomu za kugombea urais 2015 muda utakapowadia. Pia wameahidi kujichangisha
fedha kwa ajili ya malipo ya fomu hizo endapo italazimika


Share:

NATASHA GET MARRIED SOON

Hatimaye ile ndoa iliyokuwa ikusubiriwa kwa hamu kubwa na ndugu jamaa na marafiki wa mkongwe wa filamu Tanzania Suzan Lewis maarufu kama Natasha imewadia baada ya juzi kufanyiwa sherehe ya “kufundwa” kabla ya kukabidhiwa kwa mumewe hivi karibuni.

Katika habari iliyoripotiwa kwa picha na mtandao wa global publishers sherehe hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita maeneo ya  Tandika Maghorofani, Dar ambapo iliandaliwa na rafiki wa karibu  wa Natasha aliyejulikana kwa jina moja tu la Nuru.

Katika sherehe hiyo iliyohudhuriwa na mastaa wengi mavazi yalionekana kuwa ya kiasili zadi na kina dada hao kuonekana wakikata viuno vya nguvu kumpongeza Natasha

Baada ya yote hayo kukamilika, msafara wa kuelekea nyumbani kwa Natasha, Yombo ulianza huku ngoma zikiendelea kupigwa mpaka nyumbani kwa Natasha

Akizungumzia shughuli hiyo, Natasha alisema: “Nashukuru sana jamani kwa kupita hatua hii ya kwanza kuelekea kwenye ndoa yangu. Siwezi kuacha kumshukuru zaidi rafiki yangu Nuru kwa kunifanikishia.”



Share:

Updates-JOSEPH MBILINYI A.K.A SUGU AACHIWA KWA DHAMANA

MBUNGE wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi (SUGU) amekamatwa na Jeshi la Polisi Mjini Dodoma na kuachiwa kwa dhamana.

Mwandishi wetu akiwa Mjini Dodoma anasema kwamba Mbunge huyo alikamatwa muda mfupi baada ya kutoka katika vikao vya Bunge.

Sugu alikamatwa na kupelekwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Dodoma na baada ya kuhojiwa aliachiwa kwa dhamana na kutakiwa kuripoti kituoni hapo kesho asubuhi kwa mahojiano mengine.

Hata hivyo taarifa za awali za tukio la kukamatwa kwa Mbunge huyo wa Chama Cha Manedeleo na Demokrasia (Chadema) zinadai kwambwa inatokana na kosa la kutoa maneno ya uchochezi, matusi na dhihaka kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda.


Share:

Picha-CECAFA YAINGIA NUSU FAINALI

Mashindano ya kandanda ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati ya kuwania kombe la Kagame yameingia nusu fainali nchini Sudan sehemu ya Darfur Kaskazini na Kordofan Kusini.
Jumatano wiki hii Express ya Uganda inapimana nguvu na APR ya Rwanda kisha wenyeji Al Ahly Shandy dhidi ya Al Merreikh ya kutoka El Fashir, mji mdogo ambao una uwanja wa kimataifa wa ndege pamoja na viwanja vya kisasa vya voliboli, mpira wa kikapu na kandanda.
Mechi hiyo ya wenyeji inasubiriwa kwa hamu. Al Merreikh ina mashabiki wengi na wachezaji kadhaa wa nje baadhi yao Joseph Kabagambe ambaye ni mchezaji kutoka Uganda wa kiungo cha kati na Adam Williams wa Nigeria. Mchezaji mwingine wa Nigeria David Nwosu anayechezea Merreikh hatacheza kwa sababu ya kuonyeshwa kadi mbili za manjano..
Alhamisi wiki hii Vital'O ya Burundi inapepetana na Ports ya Djibouti mechi ya kwanza ya robo-fainali, na ya pili ni kati ya Rayon ya Rwanda na URA ya Uganda. Mechi za nusu-fainali ni Ijumaa na Jumamosi kisha Julai tarehe mosi ni mechi ya fainali.





Share:

WATU 37 WAFARIKI DUNIA KWENYE MGODI

Wachimba migodi 37 wameuawa baada ya mvua kubwa kusababisha kuporomoka kwa machimbo walimokuwa katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati.
Maafisa wanasema kuwa ajali hiyo ilitokea Jumapili karibu na mji wa Ndassima, umbali wa kilomita 440 Mashariki mwa mji mkuu,Bangui.
Taarifa zinazohusiana
afrika magharibi
Kwa mujibu wa msemaji wa serikali, siku tatu za kuomboleza zimetangazwa nchini humo.
Jamuhuri ya Afrika ya Kati, ina utajiri wa dhahabu na almasi lakini imekumbwa na mzozo wa muda mrefu, baada ya waasi kupindua serikali mwezi Machi.
Msemaji wa rais Prosper Ndouba, alisema kuwa anahofia kuwa watu zaidi huenda wakafariki.
"kufikia sasa idadi ya waliofariki ni 37, ingawa kuna wengi zaidi waliojeruhiwa, '' alisema bwana Ndouba
Afisaa mmoja ambaye hakutajwa jina aliambia shirika la habari la AFP kuwa idadi kubwa ya wachimbaji walikuwa kwenye machimbo hayo yaliyogeuka na kuwa tope baada ya mvua kubwa kunyesha na hivyo kuwaporomokea


Share:

Breaking News-JOSEPH MBILINYI A.K.A SUGU MBARONI

Habari zilizotufikia hivi punde zinadai kuwa Mbunge wa Mbeya mjini Mh Joseph Mbilinyi amekamatwa kwa kile kinachodaiwa ni uchochezi na kumkashifu Waziri Mkuu Mzengo Pinda.
Hivi  karibuni, Mh. Sugu  alidai  kuwa  Tanzania  haijawahi  kuwa  na  waziri  mkuu  mpumbavu  kama  Mizengo  pinda


Share:

WEMA & KAJALA PETE NA KIDOLE

Baada ya siku chache za magazeti ya udaku nchini kuripoti kuhusu kuvunjika kwa uhusiano wa karibu sana kati ya mwanadada Wema sepetu na Muigizaji mwenzake Kajala masanja, tuliamua kufanya uchunguzi wa kina ili kupata ukweli wa suala hili ili tusije kuipotosha jamii kwa habari za zisizo na ushahidi wowote.

Katika habari iliyoripotiwa na blogs na magazeti kadhaa ya udaku kuhusu kuvunjika kwa uhusiano huo zilisema kuwa chanzo ni vitendo vya mwanadada wema Sepetu “kumbania” Kajala kwenye dili anzopata za kucheza filamu na hasahasa kumkosesha dili ya kwenda china kufanya filamu aliyoalikwa na watanzania waishio nchini humo.



Bongomovies.com tuliamua kuwatafuta hewani wasanii hawa ili tuweze kupata ukweli wa jambo hili na mwanadada Kajala alikuwa wa kwanza kupokea simu na alikanusha vikali habari hizo na kuwashangaa wanaoziandika wanazipata wapi.

“Unajua mi nashangaa sana watu wanatoa wapi maneno wanayoandika, mimi sina tatizo na Wema, wala siwezi kuwa na tatizo naye, wema amekuwa msaada mkubwa kwangu, sa sijui nitagombana nini na wema, huo ni uzushi tuu jamani, muwe mnatuuliza kabla ya kuandika” Alisema kajala

Alipoulizwa kuhusu ukaribu wake mpya na wolper alisema

“Wolper nimekutana naye kwenye party ndo tukaamua kupiga picha, au siku hizi sitakiwi kupiga picha na mtu mwingine zaidi ya wema? Wolper ni rafiki yangu” Alisisitiza Kajala

 Tulipojaribu kumtafuta wema simu yake ilikuwa haipokelewi na baadaye ilipokelewa na alisema yuko location anatengeneza filamu na mwigizaji Rado hivyo tumtafute baadaye
Share: