MSANII AHUKUMIWA MIEZI 6 KWA KUIMBA MATUSI

Msanii wa kizazi kipya nchini Tunisia, Ahmed Ben Ahmed, anayejulikana kwa jina la kiusanii, Klay BBJ, amehukumiwa jela kwa miezi sita kwa kuwatusi maafisa wakuu kupitia kwa muziki wake.
Mahakama ilitupilia mbali kesi yake ya rufaa baada ya yeye na mwanamuziki mwenzake kupatikana na hatia mwezi jana ya kuwatusi maafisa wakuu katika tamasha la muziki eneo la Hammamet.
Wawili hao awali walihukumiwa bila ya wao kuwepo mahakamani kutumikia kifungo cha miezi 21 lakini hukumu hiyo iliondolewa.
Weld El 15, aliyepatikana na kosa kwa kuimba wimbo wake huo, kuwa 'Ploisi ni Mbwa', hakukata rufaa na sasa yuko mbioni.
Hata hivyo Kaly BBJ lisema kuwa wimbo wao ulikuwa unaelezea hali ilivyo nchini Tunisia na kuhusu serikali.
Muungano wa vyama unaoongozwa na chama cha wanasiasa waisilamu wenye msimamo wa kadri, Ennahda, uliingia mamlakani baada ya mapinduzi ya kiraia yaliyomwondoa mamlakani aliyekuwa rais Zine el-Abidine Ben Ali mwezi Januari mwaka 2011 na uchaguzi kufanyika baadaye mwaka huo.
Klay anasemekana kuambia mahakama kuwa wimbo wao unakosoa hali ya sasa serikalini na kote nchini Tunisia tu.
Alisema yeye ni mmoja wa wanamuziki wanaokosoa sana serikali na ndio maana wamekuwa wakimsaka sana.
Lakini majaji walikataa rufaa aliyowasilisa na kusema hukumu yake ya miezi sita gerezani inastahili kuanza mara moja.
Wakili wake alisema kuwa watawasilisha rufaa nyingine kupinga hukumu dhidi yake.


Share:

ALIYEONGOZA SHAMBULIZI KENYA KUINGIA ORODHA YA KUSAKWA ZAIDI DUNIANI

Polisi wa kimataifa Interpol, wamemuweka mwanamke aliyeshukiwa kuongoza mashabulizi ya kigaidi nchini Kenya raia Muingereza Samantha Lewthwaite, kwenye orodha ya watu wanaosakwa sana duniani.
Hatua hii ni kutokana na ombi la serikali ya Kenya kwa Interpol.
Bi Lewthwaite, mwenye umri wa miaka 29, ni mjane wa mlipuaji aliyefanya shambulizi la kujitoa mhanga mjini London Uingereza mwezi Julai mwaka 2005
Anajulikana kama "white widow", na amehusishwa na kundi la kigaidi la Al Shabaab nchini Somalia.
Polisi wa Interpol hata hivyo hawakuhusisha hatua ya kumsaka Samantha na shambulizi la kigaidi dhidi ya jumba la maduka la Westgate mjini Nairobi lililowaua watu 67.
Hata hivyo, hatua hii ya kumsaka Bi Lewthwaite inakuja punde baada ya shambulizi hili la kigaidi nchini Kenya.
Al-Shabab ilikiri kufanya mashambulizi hayo yaliyotokana na kutekwa kwa jengo la Westgate na kisha kutekwa kwa raia wa kawaida waliokuwa ndani ya jengo hilo kwa siku nne.
Kwa mujibu wa polisi wa Interpol, mwanamke huyo anasakwa na serikali ya Kenya kwa kumiliki mabomu na kupanga njama ya kufanya mashambulizi kuanzia Disemba mwaka 2011.
Ikiwa mwanamke huyo atakamatwa katika nchi mwanachama wa Interpol, atazuiliwa na kusibiri kupelekwa katika nchi anayotakikana kwa kesi kufunguliwa dhidi yake.
Bi Lewthwaite anajulikana kwa jina bandia la, "Natalie Webb" –na alikuwa anasakwa kwa madai ya kumiliki hati bandia ya usafiri nchini Afrika Kusini.
Ni mjane wa Germaine Lindsay, mmoja wa washambuliaji wanne waliohusika na shambulizi la kigaidi mjini London ambapo watu 52 waliuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa


Share:

SHAMBULIZI LINGINE KENYA

Kuna taarifa za kikundi cha magaidi wa Al-Shabab kuvamia kituo cha polisi katika mji mdogo wa Mandera uliopo mpakani mwa Kenya na Somalia.

Shambulizi hilo ambalo limefanyika mapema leo limesababisha vifo vya polisi wawili na wengine kadhaa kujeruhiwa, huku magaidi hao wakichoma moto magari 11.

Duru za kiuchunguzi zinaonesha kwamba hiyo ni sehemu ya mfululizo wa mashambulizi yaliyoandaliwa na Al-Shabab baada ya lile la Westgate, jijini Nairobi.


Share:

MATEKA 137 WADAIWA KUUWAWA NA AL SHABAAB

Kundi la Al-Shabaab limedai siku ya Jumatano kuwa mateka 137 waliowachukua wamekufa katika uvamizi wa kituo cha biashara, idadi ambayo ni vigumu kuithibitisha na kubwa kuliko idadi iliyotangazwa kuwa hawajulikani walipo.

Wapiganaji hao walio na mafungamano na mtandao wa Al-Qaeda, katika ujumbe waliouweka katika mtandao wa kijamii wa twitter, walisema mateka 137 waliokuwa wanashikiliwa na mujahedeen walikufa. Waliwashtumu pia wanajeshi wa Kenya kwa kutumia vifaa vya kemikali kukomesha mkwamo huo uliodumu kwa siku nne. "Katika hatua ya uoga wa dhahiri, vikosi vya Kenya kwa maksudi vilitumia vilipuzi vilivyokuwa na kemikali," ulisema ujumbe mmoja na kuongeza kuwa, "ili kufunika uhalifu wao, serikali ya Kenya iliendesha zoezi la kuliporomosha jengo, na kuuzika ushahidi na mateka wote chini ya vifusi."
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, alitangaza kumalizika kwa umwagaji huo wa damu uliodumu kwa saa 80 jioni ya Jumanne, ambao ulisababisha vifo vya raia 61 na maafisa sita wa vikosi vya usalama. Polisi ilisema idadi hiyo ya vifo ingeweza kuongezeka, ambapo shirika la misaada la Msalaba mwekundu liliorodhesha watu 63 ambao bado hawajulikani walipo. Hakukuwa na kauli kutoka serikali ya Kenya kuhusiana na madai hayo, lakini Al-Shabaab wamekuwa wakitoa madai ya ajabu huko nyuma, hasa kupitia akaunti yao kwenye mtandao wa twitter.
 Wanajeshi wa ulinzi wa Kenya wakijiandaa kuingia jengo la Westgate kupambana na wavamizi. Wanajeshi wa ulinzi wa Kenya wakijiandaa kuingia jengo la Westgate kupambana na wavamizi.
Kundi hilo lilisema lilifanya shambulizi hilo katika kulipiza kisasi dhidi ya Kenya kutokana na kujiingiza nchini Somalia kupambana na wanamgambo hao. Katika moja ya mashambulizi mabaya zaidi katika historia ya Kenya, wapiganaji hao waliingia katika jengo la maduka la Westagate lenye ghorofa nne, ambalo linamilikiwa kwa sehemu na raia wa Israel, mchana wa Jumamosi, na kuanza kuwashambulia wanunuzi kwa risasi na kuripua maguruneti.
Kenya ilianza siku tatu za maombolezi rasmi Jumatano, ambapo bendera za taifa zinapepea nusu mlingoti, huku wafanyakazi wa uokozi wakisafisha mabaki ya jengo la Westgate kutafuta miili ya wahanga wa tukio hilo. Karibu watu 200 walijeruhiwa katika uvamizi huo wa siku nne, ambao ulishuhudia mapambano makali kati ya wapiganaji na vikosi vya usalama vya Kenya katika jengo hilo, ambalo ndicho kituo kikubwa zaidi cha biashara na maarufu kwa watu wenye uwezo nchini Kenya, wanadiplomasia, wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na watalaamu wengine.
Raia wa Uingereza akamatwa
Wakati huo huo, raia wa Uingereza alikamatwa mjini Nairobi kufuatia shambulio hilo, ofisi ya mambo ya kigeni ilisema Jumanne mjini London. Kwa mujibu wa gazeti la kila siku la Daily Mail, raia wa Uingereza mwenye umri wa miaka 35 mwenye asili ya Somalia, alikamatwa katika uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta wakati akijaribu kuondoka nchini Kenya kwa ndege ya Uturuki.
Msemaji wa Ofisi ya mambo ya kigeni alikataa kuzungumzia ripoti hiyo, akisema serikali ya Uingereza ilikuwa inafahamu juu ya kukamatwa kwa Muingireza huyo, na ilikuwa tayari kutoa msaada wa kibalozi. Chanzo kutoka idara ya kupambana na ugaidi katika jeshi la polisi la Kenya kililiambia shirika la habari la Reuters kuwa raia wa Uingereza mwenye asili ya Somalia alikamatwa na kuzuiwa katika uwanja wa ndege baada ya kukosa ndege yake, na kwamba alikuwa anahojiwa. Lakini hakikutoa taarifa zaidi.
 Moshi ukifuka kutoka jengo la Westgate. Ghorofa tatu za jengo hilo ziliporomoka. Moshi ukifuka kutoka jengo la Westgate. Ghorofa tatu za jengo hilo ziliporomoka.
Gazeti la Daily Mail lilisema kuwa mwanamume huyo alizua wasiwasi uwanjani kwa sababu alikuwa na jeraha usoni mwake, alikuwa amevaa miwani myeusi, na mwenendo wake ulikuwa unazua mashaka. Gazeti hilo lilisema kuwa hati ya kusafiria ya mwanamume huyo ilionekana kuwa halali na ilikuwa na viza ya Kenya, ingawa hakukuwa na mhuri wa kuonyesha lini na vipi aliingia nchini Kenya.
Uganda yasema vita dhidi ya Al-Shabaab bado vigumu
Mkuu wa majeshi ya Uganda Jenerali Katumba Wamala alisema vikosi vya Umoja wa Afrika vinavyopambana na Al-Shabaab nchini Somalia vinakabiliwa na changamoto za uwezeshwaji, na kwamba vinaweza visimalize operesheni yake katika muda uliopangwa kutokana na kutokuwa na vitendea kazi vya kutosha, anaripoti mwandishi wa DW mjini Kampala, Leylah Ndinda. Katumba alisema kwa sasa hawawezi kuingia katika maeneo mapya wanakojificha al-Shabaab kutokana na ukosefu wa vitendea kazi na hata upungufu wa wanajeshi, na kwamba tayari wamekwisha wasiliana na Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa kuhusiana na changamoto hizi.
Jenerali Katumba Wamala alisema pamoja na ukweli kwamba kikosi cha Umoja wa Afrika nchini Somalia, AMISOM, kinaweza kuendelea na operesheni zake, inawezekana wakachukua muda mrefu kuliko ilivyotarajiwa. Mataifa yanayochangia wanajeshi nchini Somalia, yalisema kuwa yalitaka kuondoka nchini humo ifikapo mwaka 2016. Mkuu huyo wa majeshi ya Uganda, UPDF, sasa anapendekeza kuwa kama Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa hawawezi kuiwezesha AMISOM, basi wajikite katika kutoa mafunzo kwa jeshi la Somalia, na kutumia raslimali zilizopo kuwalipa mishahara.
 Mkuu wa jeshi la Uganda, UPDF, Jenerali Katumba Wamala. Mkuu wa jeshi la Uganda, UPDF, Jenerali Katumba Wamala.
Akizungumzia uvumi kuwa AMISOM inaweza kugeuzwa kuwa kikosi cha Umoja wa Mataifa, Jenerali Wamala alisema kulingana na uzoefu wa huko nyuma, Wasomali wanawaamini sana wanajeshi wa Afrika kuliko wa Umoja wa Mataifa. Uganda ndiyo ilikuwa nchi ya kwanza kupeleka wanajeshi wake nchini Somalia, ikitumai kuwadhoofisha wapiganaji wa Al-Shabaab katika kipindi cha muda mfupi.
Polisi Burundi yazingira mitaa ya Waislamu
Naye Mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya DW mjini Bujumbura, Amida Issa, anaripoti kuwa polisi ya taifa ya Burundi iliuzingira mtaa wa Buyenzi mjini Bujumbura na Rumonge mkoani Bururi alfajiri ya Jumatano, katika kile ilichosema ni kuwasaka wapiganaji wa Al-Shabaab na wanaowaunga mkono. Mitaa hiyo yote ina wakaazi wengi ambao ni Waislamu. Burundi ni miongoni mwa mataifa yaliyo na wanajeshi wake nchini Somalia.


Share:

HIVI NDIVYO PANYA WANAVYOTUMIKA KUGUNDUA MABOMU ARDHINI

Shirika moja lisilo la kiserikali la Ubelgiji APOPO limeanza kuwafundisha panya namna ya kutambua mabomu yaliyofukiwa ardhini. Panya hao ambao ni wakubwa kuliko panya wa kawaida wanafanyiwa majaribio Morogoro Tanzania .Inaaminika wanauwezo mkubwa wa kunusa kuliko mbwa. Hii inatokana na kuwa pua zao zipo karibu na ardhi,hali ambayo inawasaidia katika kazi yao ya utambuzi wa mabomu.


Panya wanafundishwa jinsi ya kunusa wakiwa wadogo, kwa kuwekewa vitu vyenye madini ya milipuko.Tangu mwaka 2000, APOPO imekuwa ikiwafunza panya kwenye chuo cha Sokoine,Morogoro. Mwaka 2006 panya wa hao walianza zoezi la kutafuta mabomu ya ardhini huko Msumbiji. Kabla ya panya kuanza kazi ya kunusa wapi mabomu yalipo, lazima wafuzu mtihani kutimiza viwango vya kimataifa vya kutambua mabomu ardhini.


Panya hujifunza kufuata eneo fulani hatua kwa hatua. Waya au kamba hufungwa mwilini kutoka kwenye ufito. Wasimamizi wawili husimama kila upande wa ufito na kumruhusu panya kutembea toka mwanzo wa ufito hadi upande mwingine kwa kufuata jinsi waya au kamba alizo fungwa mwilini. Katika mafunzo ya awali panya hufunzwa kunusa kemikali aina ya TNT ndani ya chombo cha chuma


Baadaye kila panya hufanya mafunzo kwenye eneo ambalo kuna mabomu ya ardhini yaliyofukiwa na vifaa ambayo huzuia mlipuko. Ikiwa panya ameweza kunusa na kutambua yalipo madini asilia ya TNT huwa anasimama na kuanza kufukua sehemu hiyo ya ardhi iliyofukiwa bomu. Kuwafundisha panya kunachukua muda wa mwaka na inagharimu dola za Kimarekani $6,000 sawa na Euro 4,670



Wakati wa mafunzo panya hupewa zawadi kwa kufuzu vizuri kwa sauti maalumu ambayo inaashiria kufuzu kwake na kupewa kipande cha ndizi kama zawadi. Panya aliyefuzu vizuri huwa ana uwezo wa kuzunguka mita 400 za mraba kwa siku, wakati eneo kama hili litamchukua binadamu wiki mbili ili kuweza kugundua wapi kumefukiwa bomu



Kulinganishwa na mbwa, panya wanaweza kutumiwa na mtu yeyote kwani hawana tabia ya kutokuwa na mahusiano ya karibu na mtu aliyemfundisha kama walivyo mbwa. Panya anaweza kufanya kazi ya kufichua mabomu, hata kama aliyemfundisha hayupo na huwa wanafanya kazi vizuri kwa ufanisi na mtu yeyote. Hakuna shida kwa panya aliyefundishwa Tanzania, kwenda kufanya kazi Msumbiji, Angola,Thailand na Kambodia



Hadi kufukia sasa nchini Msumbiji, zaidi ya mita za mraba milioni 6,5 za ardhi zimeshachunguzwa na mabomu 2,000 yaliyotegwa ardhini yamepatikana na kuharibiwa, pia bado mabomu 1,000 kuteguliwa na bunduki na silaha nyingine ndogo 12,000 zilipatikana. Na mpaka sasa kuna makundi saba yenye watu 54 ambayo yanashughulika na kazi ya kutegua mabomu kwa kuwatumia panya


Share:

ANGALIA SHULE INAYOJENGWA JUU YA MAJI

Watoto katika wilaya ya Makoko laazima wajifunze kuogelea ikiwa wanataka kwenda shuleni. Kwa sababu wilaya hiyo katikati mwa mji mkuu wa Nigeria Lagos imekumbwa na mafuriko tangu mwezi Machi 2013. Shule inayoelea ni mfano wa usanifu majengo wa kiafrika "Afritecture". Usanifu huu unaweka kando dhana za ujenzi wa kimagharibi na kutegemea zaidi mbinu za kienyeji na vifaa kama vile mbao.


Share:

(SOMA) MWANADADA ASIMULIA ALIVYOJIOKOA KUTOKA WEST GATE

Sneha Kothari Mashru ni mwanadada mtangazaji wa redio ambaye alikuwa ndani ya jengo wakati tukio linatokea.Asimulia jinsi alivyojiokoa kutoka ndani ya jengo hilo wakati kijana aliyekuwa karibu nae akiwa amepigwa risasi na kufariki.

Asimulia kuwa alitumia damu za watu waliojeruhiwa na waliokufa kujipaka mwilini mwake ili kuonyesha magaidi kuwa na yeye ni moja ya watu walioaga dunia ndani ya jengo.

Kitu cha kwanza alizima simu yake ili isiweze kutoa sauti ikiwa itatokea kuita ili kutowashitua magaidi na kupelekea kupoteza maisha yake.

SOMA HAPA CHINI ALIVYOELEZEA.....

"I realised he was shot, because he was bleeding," she said.

"So I pulled out (his) phone slowly and I tried to switch it off, it was all full of blood, and I tried to switch off the phone so that it could stop ringing (in case it alerted the attackers).

"So I took a lot of his blood, (as) much (as) I could and I tried to put it on myself. I put it on my arm, a lot of the teenager's blood, and while I was trying to put it on my hand I just realised that he had stopped breathing at that time.

"So I put it on my arm, as much as I could, and I covered my face with my hair, because my hair was let loose even then, just to pretend that I'm dead or probably badly injured.

"I would still love to know who he is and everything, because his blood probably protected me from getting probably more injured or attacked."


Share:

MWANDISHI WA VITABU,MTANGAZAJI, MPWA WA KENYATA,MFANYAKAZI WA BENKI YA BARODA WAFARIKI KATIKA SHAMBULIZI

Takriban watu 62 wameuawa kwenye mashambulizi ya kigaidi nchini Kenya dhidi ya jengo la kifahari lenye maduka zaidi ya themanini la Westgate.


Ruhila Adatia-Sood


Ruhila Adatia-Sood na mumewe Ketan Sood Ruhila Adatia-Sood walioana tu mwezi Januari mwaka jana.
Ruhila, alikuwa katika ghorofa ya juu ya duka la Westgate ambako alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wameandaa mashindano ya upishi kwa watoto.
Alikuwa ameolewa na Ketan Sood, aliyefanya kazi na shirika la USAid mjini Nairobi mwezi Januari mwaka 2012,na harusi yake ilitajwa kuwa harusi ya kiswahili ambayo ilisherehekewa kwa siku tatu.
Alikuwa mjamzito na mimba ya miezi sita alipofariki.
Kulingana na ripoti Adatia-Sood alikimbizwa hospitalini , lakini alifariki baada ya kuwasili kutokana na kuvuja damu nyingi.
Alisifika kote nchini kwa moyo wake mzuri wa kuwafanya watu kutabasamu daima.

Polisi wakikabiliana na wanamgambo hao waliokuwa wameteka jengo la Westgate
Kwenye ukurasa wake wa Twitter alijitaja kuwa mpenda chakula na mtu mwenye kufurahia michezo ya kusisimua.
Alisomea katika chuo kikuu cha Rhodes nchini Afrika Kusini , na dada zake watatu wamemtaja kama mtu mwenye ari kubwa maishani.
Pia alikuwa mtangazaji wa kituo cha redio cha East FM na pia alitangaza habari kwenye kituo cha televisheni ya Kiss.
Magaidi waliwarushia magurunedi Rahila na mtangazaji mwenzake pamoja na watoto waliokuwa ndani ya jengo hilo lakini Ruhila hakuponea. Mwenzake Kamal Kaur, pia mtangazaji wa redio alikuwa ameambatana na watoto wake ambao walifyatuliwa risasi ingawa ziliwakosa na kumgonga mtoto aliyekuwa karibu nao. Wao walijeruhiwa miguuni.
Kaur na wanawe walifanikiwa kukimbilia usalama wao

.
Mbugua Mwangi and Rosemary Wahito

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pia aliwapoteza jamaa zake katika shambulizi hilo. Mbugua Mwangi ni mpwa wa Kenyatta na alikuwa na mchumba wake Rosemary Wahito wakati waliposhambuliwa kwa risasi na kuuawa papo hapo.
Akihutubia taifa, Kenyatta alisema kuwa, "ninamuomba Mungu awape utulivu wakati sote tukikumbwa na msiba huu na ninajua mnachokihisi hasa ikiwa umempoteza jamaa wako katiakshambulizi hili baya.''
Kulingana na taarifa ya jarida la nchini Ireland, mamake Mwangi, Catherine Muigai Mwangi, ndio alikuwa tu amerejea kutoka Dublin ambako alikuwa balozi wa Kenya kwa miaka sita .
Dadake mkubwa Rais Kenyatta Christine Wambui Pratt pia alikuwa katika jengo hilo lakini alifanikiwa kunusuru maisya yake.


Mitul Shah


Mitul Sha alipenda sana soka
Mitul Shah Mitul Shah alikuwa mkuu wa timu ya soka ya kampuni yake ambayo inacheza katika divisheni ya pili.
Afisaa mkuu mtendaji wa mauzo katika kampuni ya Bidco, ambayo hutengeza mafuta ya kupikia, Mitul Shah alikuwa katika ghorofa ya juu zaidi ya jengo hilo.
"Alifariki akijaribu kuwaokoa watoto waliokuwa wamekwama ndani ya jengo hilo. Kwa marafiki wa Mitul, alifariki kama shujaa .
Rafiki zake wamemtaja kama shabiki sugu wa Manchester United.
Pia alikuwa mwenyekiti wa timu ya soka ya Bidco.



Joyti Kahrmes Vaya na Maltiben Ramesh Vaya
Joyti Kharmes Vaya alikuwa na umri wa miaka 37 mwenye watoto watatu, ambaye mumewe alifanya kazi katika benki ya Victoria Commercial bank.
Maltiben Ramesh Vaya alikuwa na miaka 41 , mama wa watoto wawili aliyefanya kazi katika Benki ya Baroda.
Wawili hao walikufa kutokana na majeraha waliyopata, kutoka na risasi



Kofi Awoonor


Raia wa Ghana mwenye umri wa miaka 78 malenga anayesifika sana. Anasifika nyumbani kwao kama mwandishi ambaye vitabu vyake vinatumiwa katika shule nyingi nchini Ghana.
Alikuwa mjini Nairobi kushiriki hafla ya Storymoja na alitarajiwa kutumbuiza watu siku ya Jumamosi.
Alisifika kwa nyimbo na mashairi yake mapema miaka ya sitini.
Miaka ya sabini alifunza katika baadhi ya vyuo vikuu nchini Marekani na kurejea Ghana mwaka 1975 kuchukua wadhifa wa mwalimu wa lugha ya kiingereza katika chuo kikuu cha Cape Coast.
Katika muda wa miezi kadhaa, alikamatwa na kuzuiliwa kwa madai ya njama ya uhaini wakati wa utawala wa kijeshi wa Kanali Ignatius Acheampong.
Mwanawe Awoonor alikuwa naye wakati wa shambulii hilo mjini Nairobi na alipigwa risasi mkononi wakati wa shambulizi hilo
Share:

BINGWA WA NGUMI(MASUMBWI) AFARIKI DUNIA


Bingwa wa zamani wa dunia katika ndondi uzani wa Heavyweight mmarekani Ken Norton amefariki akiwa na umri wa miaka 70
Anakumbukwa zaidi kuwa kumshinda gwiji wa masumbwi Mohammad Ali mwaka 1973.
Sawa na mabondia wengi wa uzani mkubwa enzi zake, Ken Norton anakumbukwa kwa jinsi alivyopigana na Mohamed Ali.
Na kwenye pigano lao la kwanza la mwaka 1973, Norton ambaye hadi wakati huo hakujulikana sana alimkomesha Ali na kumshinikiza makonde tangu mwanzo hadi mwisho.
Norton alivunja taya la Ali kwenye pigano la raundi 12, akawa bondia wa pili kumshinda Mohamed Ali tangu alipoanza ndondi za kulipwa.
Katika mapigano yaliyofuatia, baadaye mwaka huo wa 73, Ali alilipiza na kumshinda Norton, na TENA mara nyingine miaka mitatu baadaye kwenye pigano lao la mwisho katika uwanja wa Yankees, mjini New York. Lakini hata hivyo Norton baadaye alitwaa taji la ulimwengu la WBC, kabla ya kulipoteza kwa Larry Holmes mwaka 1978.
Norton, bingwa wa Marekani uzani wa Heavyweith alikuwa ameanza mchezo wa ndoni mwaka wa 63 akiwa katika jeshi la wanamaji. Lisilosahaulika daima ni pigano hilo la mwaka 73 alipomshinda kumshinda Mohammed Ali, akimvunja taya. Alistaafu masumbwi mwaka wa 81.
Alishiriki mapigano 50 ya ndondi za kulipwa, na afya yake ikadorora ingawa alikataa kuulaumu mchezo wa masumbwi kama sababu ya maradhi yake. Alitatizwa na ugonjwa wa kiharusi mara kadhaa. Afya yake imemsumbua kwa mda hadi kufariki kwake akiwa mwenye umri mdogo wa miaka 70



Share:

HUYU MWANAMKE MUINGEREZA ASHIRIKI KUSHAMBULIA WESTGATE

Samantha Lewthwaite N i mwanamke mwenye asili ya uingereza ambaye ametajwa kuhusika na shambulio la westgate nchini kenya mapema wiki hii.Huyu ni mwanamke mjane ambaye inasemekana yupo East Afrika na alikuwa anatafutwa na askari Wa kenya kwa kupanga mashambulizi kadhaa ambayo alijaribu kufanya katika nchi kadhaa za mwambao.(coast country)


Share:

MAGAIDI 3 WAUWA,ASKALI 11 WA KENYA WAMEJERUHIWA

Taarifa za hivi karibuni kutoka kwa msemaji wa jeshi la kenya KDF zinasema kuwa askali 3 wanaosadikiwa kuwa ni magaidi wameuwa na jeshi lake.Pia ametoa taarifa kuwepo kwa majeruhi 11 wa jeshi lake KDF.

Aliongeza tena kutoa takwimu za watu waliookolewa kutoka katika jengo hilo ambao idadi yake hakuitaja kamili zaidi alisema ni zaidi ya 62.


Raia 11 wanashikiliwa na jeshi hilo kwa mahojiano zaidi,huku milio ya risasi ikiendelea kusikika katika eneo la tukio.


"Kenya Defence Forces ( KDF) has reported that three terrorists have been killed and 11 Kenyan soldiers injured in the Westgate operation that has lasted for over 48 hours"


Share:

(Picha) MOSHI UKIWA UNATOKA KATIKA JENGO LA WEST GATE

Mchana wa leo eneo la West gate kumeonekana moshi mzito ukiwa unavuka kutokea ndani ya jengo lililoshambuliwa jana na kikundi cha kigaidi cha Al shabaab nchini kenya.Kwa mujibu wa BBC wanasema wanajeshi wa Kenya walilipua mabomu  ili kuendelea kukabiliana na tukio hilo.Pia mpaka sasa inasemekana watu waliofariki yafikia 69 na na wengine mamia wamejeruhiwa huku idadi isiyojulikana wakiwa wameshikiliwa mateka na Al Shabaab!!



Share:

HII NDIYO SABABU YA AL SHABAAB KUPIGA WESTGATE

Katika mahojiano yaliyofanyika hivi karibuni baada ya tukio la mashambulizi nchini Kenya katika sehemu ya kibiashara ya westgate mall,kiongozi wa al shabaab amesema sababu za wao kuamua kushambulia eneo hilo.

".....ni kwa sababu sehemu hii inaingiza pesa nyingi na ipo katikati ya jiji.Ni sehemu wanasikia maumivu na tulitaka ujumbe ufike......."


HILI NDILO JENGO LILILOSHAMBULIWA NA AL SHABAAB NCHINI KENYA
Share:

POST HII YA NEY WA MITEGO YALETA UTATA

Hii ni post ambayo imepata comment nyingi ikiuliza kuwa amepata msiba wa nani?


Share:

AL SHABAAB WAJITAJA KUHUSIKA NA SHAMBULIZI KENYA

Afisaa mmoja mkuu wa kundi la kigaidi la Alshabaab, amefahamisha BBC kuwa kundi hilo ndilo limehusika na shambulizi dhidi ya duka la kifahari la Westage mjini Nairobi Kenya.
Kwa mujibu wa Afisaa huyo mashambulizi hayo yalikuwa ya kulipiza kisasi kwa Kenya kwa kujihusisha na vita vya Somalia ambako wanajeshi wake wanakabiliana na kundi hilo.
Wanajeshi wa Kenya wamekuwa nchini humo tangu mwaka 2011 kama sehemu ya juhudi za muungano wa Afrika kutaka kurejesha uthabiti nchini Somalia.
Afisaa mkuu wa mambo ya ndani Kenya amesema idadi ya waliofariki ni kumi na moja lakini shirika la msalaba mwekundu linasema idadi hiyo imefika watu 30 huku zaidi ya hamsini wakijeruhiwa.
Taarifa kutoka Ikulu ya Rais Kenya zinasema kuwa mshukiwa mmoja aliyekamatwa alifariki kutokana na majeraha yake.

Baadhi ya watu waliofanikiwa kukimbilia usalama wao
Wanamgambo wa Al Shabaab kupitia kwa mtandao wao wa Twitter , wanasema kuwa Kenya haikuchukulia kwa uzito onyo walilotoa kwa taifa hilo kwa hatua ya kuwapeleka wanajeshi wake nchini humo kupambana dhidi yao.
Kundi hilo limesema limekuwa likitoa onyo mara kwa mara kwa Kenya kuwa ikiwa haitaondoa vikosi vyake nchini Somalia, athari zitakuwa mbaya mno.
Kupitia mtandao wao wa Twitter, Al Shabaab limesema kuwa Kenya ilijidai kutosikia onyo hizo, na kuendelea kuwaua waisilamu wasio na hatia nchini Somalia.
Taarifa hiyo ya Twitter ilisema kuwa Shambulio la Westgate ni tone tu katika bahari ya mfano wa yanayowakumba wasomali nchini Somalia.
Taharuki ilianza hii leo saa saba mchana wakati watu wanaokisiwa kuwa kumi walipovamia jengo la kifahari la Westgate la kuwapiga risasi kiholela wakenya waliokuwa wanaendelea na shughuli zao za kawaida.
Kwa mujibu wa shirika la msalaba mwekundu , takriban watu 30 walifariki kwa kupigwa risasi au kutokana na majeraha yao na wengine wengi wenye majeraha ya risasi kukimbizwa hospitalini kwa matibabu.














Share:

WAISLAM WAPINGA MISS WORLD KUFANYIKA INDONESIA

Waislamu kutoka nchini Indonesia wamepiga vita kufanyika mashindano ya dunia ya urembo nchini humo.Kikundi kimoja cha kiislamu kinachoitwa  Indonesian hard line Islamic group kilifanya maandamano makubwa kupinga swala hilo kufanyika ndani ya nchi hiyo na kukiita kitendo hicho kuwa ni ukafiri.
Maandamano hayo yamefanya kuhairishwa kwa mashindano hayo kufanyika Jarkata nchini humo na kutarajiwa kufanyika BALI nje kidogo ya mji wa Jarkata mwishoni mwa mwezi huu tarehe 28/9/.








Share:

ROBIN VAN PERSIE- "NAPENDA KUSIKILIZA NYIMBO ZA P SQUARE"

Mshambuliaji machachali wa Manchester United,Robin Van Persie amesema kuwa kati ya vitu anavyopenda wakati akiwa nyumbani kapumzika ni kusikiliza muziki.Alipoulizwa ni aina gani ya muziki ambao anapenda kusikiliza,moja ya watu aliowataja ni wanamuziki kutoka nigeria P Square

Nukuu  alijibu hivi

 “I like to listen to music. ..all sorts honestly. I can listen to Dutch songs, English songs..whatever…if the tune is good I like it… Michael Jackson, Usher, P-Square…all sorts honestly.”




Share:

BREAKING NEWS - ELBORU SEKONDARI YAFUNGWA

 Shule ya Sekondari Ilboru, imefungwa na serikali kufuatia tishio la kuchomwa moto, kutokana na mgogoro wa wanafunzi na waalimu. Wanafunzi 4 wanahojiwa, 800 wamerudishwa nyumbani
Share:

(PICHA) WILLIAM RUTO AKIWASILI MAHAKAMA YA KIMATAIFA

Ile kesi inayokabili makamu wa raisi wa Kenya bwana william Ruto inaendelea kusikilizwa katika mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai ICC.

Deputy President Wiliam Ruto is welcomed to ICC in the Hague by his lawyer Karim Khan. The case had been adjourned.












Share: