MSAFARA WA OBAMA - MAMA AKAMATWA AKIKATIZA BARABARANI

Maafisa Usalama waliokuwa wamejichanganya na wananchi, walimkamata mama mmoja aliyekuwa akijaribu kuvuka barabara kabla ya msafara wa Rais Jakaya Kikwete kupita wakati akienda kumpokea mwenyeji wake, Rais Obama.

Kwa kuwa kila mmoja alikuwa akimwangalia, wakati anajiandaa kukatisha barabara na msafara unakuja, walimkimbilia na kumdaka na kisha kuondoka naye. Hata hivyo haikuweza kufahamika mama huyo alikuwa na lengo gani.
Share: