MAELEZO KUHUSU KIFO CHA MANGWAIR

KIFO CHA ALBERT MANGWAIR 28/May/2013, R.I.P!!!

HABARI KUTOKA KWA SAICO DOS

HABARI ZINASEMA KUWA alikuwa yeye na wenzake 3 yani walikuwa wa 4, Leo asubuhi walikuwa wanarudi Brixton wakitokea town Johanessburg,Ngwair tiketi yake ya ndege ilikuwa tayari kwa ajili ya safari Leo hii hivyo tulikuwa tayari kumsindikiza Airport Leo Asubuhi, hvyo wakamgongea mlango mshikaji akawafungulia, waliingia ndani lakini walikuwa wamelewa, sasa ikawa wanaendelea kula mambo yao ndani,ghafla Mangwair akaanza kujisikia vibaya, then akaanguka chini na kupoteza faham wakaona kama anafanya masihala, hali hiyo iliendelea hadi mida ya saa sita mchana ikawa mbaya zaidi pia jamaa mwingine nae akapoteza fahamu hvyo hvyo coz walizidisha mambo kutumia,tukaitwa kumchek ikabd tuogope mpaka mida ya saa nane mchana ilibd tumpigie simu jamaa fulan Msouth Africa ni Taxi Driver ili tumpeleke Hospital coz sis tuliogopa kumpeleka na magar yetu Binafsi, akaja tulimchukua pamoja na yule mwingne had hospital kufika kule Doctor kumchek alikuwa tayar ameshakufa na yule mwingne bado yu hai ila hali yake sio nzur, ilibd jamaa Kat yetu aka sign kuhusiana na kufa kwa Albert Mangwair hvyo kesho Doctor atatupatia karatas ili tukabdhiwa mwili wake kwa ajr yakuusafirisha Tanzania!! Hivyo Ndvyo ilivyokuwa had kufa kwa Albert Mangwair mwili wake upo Helen Joseph Hospital in Hursthill next to Aukland park and University of Johannesburg, also Brixton and Westdene in Johannesburg South Africa!!
Share: