AFYA YA MANDELA YA YAHIMARIKA

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, amesema kuwa
 amefahamishwa na madaktari wanaomtibu kuwa, hali
ya Mzee Mandela ambaye
anaendelea kupokea
 matibabu katika hospitali
moja mjini Pretoria imeimarika.Siku ya Jumanne rais Zuma, alisema
 kuwa nchi yote inazidi kumwombea Mzee Nelson
 Mandela ili apate afueni haraka.Rais Zuma
amesema amefurahishwa na jinsi hali ya rais huyo
 inavyoendelea kuimarika, baada ya kudhohofika sana siku chache zilizopita.
Rais huyo wa zamani amelazwa hospitalini
 Pretoria, ambako anatibiwa maambukizi ya mapafu.
Katika taarifa yake rais Zuma amesema japokuwa
 Mandela ameathirika sana, madaktari
 wanaomshughulikia wanafanya kazi nzuri.
Rais huyo mstaafu wa Afrika Kusini, amelazwa
hospitalini kwa siku ya tano leo ambako
anapokea matibabu ya ugonjwa wa mapafu

Share: