OSTAZ JUMA NA MUSOMA AJA NA NGOMA MPYA "MUZIKI KAZI"

Mmiliki wa lebo ya watanashati entertainment Ostaz Juma na Musoma ameamua kuingia studio na kutengeneza ngoma akiwa amemshirikisha Young killa.Ngoma hiyo aliyoipa jina la muziki kazi ambayo ameifanyia Mwanza kwenye studio za K Records.Ostaz alisema kuwa alipofika katika studio hizo alikutana na young killa ndipo waamua kuweka mawazo ya kufanya ngoma hiyo.
Pia Ostaz alisema kuwa amefunikwa na YOUNG KILLA katika wimbo huo kutokana na uzoefu wa kazi hiyo.

Wimbo huo unatarajiwa kutoka baada ya mwezi huu mtukufu na utaachiwa kwenye internet peke yake.

KAA TAYARI.

MSIKILIZE HAPA ALICHOKISEMA OSTAZ JUMA NA MUSOMA.


Share: