SHAMBULIZI LINGINE KENYA

Kuna taarifa za kikundi cha magaidi wa Al-Shabab kuvamia kituo cha polisi katika mji mdogo wa Mandera uliopo mpakani mwa Kenya na Somalia.

Shambulizi hilo ambalo limefanyika mapema leo limesababisha vifo vya polisi wawili na wengine kadhaa kujeruhiwa, huku magaidi hao wakichoma moto magari 11.

Duru za kiuchunguzi zinaonesha kwamba hiyo ni sehemu ya mfululizo wa mashambulizi yaliyoandaliwa na Al-Shabab baada ya lile la Westgate, jijini Nairobi.


Share: