RUVUMA-WATU 8 WAMEFARIKI DUNIA KWA AJALI

Watu nane wamefariki dunia  baada ya gari walilokuwa wanasafiria kutoka kijiji cha mputa wilaya ya Namtumbo kwenda Songea  kuacha njia na kupinduka katika kijiji cha Hanga eneo la Bombambili wilaya ya Namtumbo mkoa wa Ruvuma .
Roli hilo lilikuwa limebeba magunia ya ufuta, mpunga wakiwemo na abiria

 Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma  Deusdedit  Nsimeki amesema ajali hiyo imetokea jana Tarehe 26.05.2013 majira ya saa nne na nusu( 4:30 usiku  katika kijiji cha Hanga eneo la bombambili mkoa wa Ruvuma, chanzo cha ajili hiyo ni mwendokasi na dereva kuendesha gari akiwa amelewa,

Ajali hiyo  imehusisha gari lenye namba za usajili T.677 ADL  aina ya Isuzu lori , mali ya mfanyabiashara wa mazao maarufu kwa jina la Mtazamo. likiendeshwa na dereva aitwae CHRISTIN NYONI mwenye umri wa miaka 30, mkazi wa LIHULI SONGEA,
Baada ya ajali hiyo kutokea dereva wa gari hilo amekimbia na kutelekeza gari porini hadi sasa jeshi la Polisi mkoani Ruvuma linafanya jitihada za kumtafuta ili sheria ifuate mkondo wake.

Kamanda wa Polisi amesema gari  hilo liliacha njia baada ya kugonga daraja na kupinduka na kusababisha vifo vya watu nane(8)  na majeruhi kumi na moja (11) ambao
wote wamelazwa katika hospitali ya Mkoa wa Ruvuma kwa matibabu.


Kutokana  na ajali hiyo mbaya kamanda wa polisi wa  Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimeki ametoa wito kwa wamiliki wa magari ya mizigo kutopakia mazao pamoja na abiria na atakayekiuka atachukiliwa hatua kali za kisheria.
Pia ametoa wito kwa wamiliki/wasimamizi wa magari kuwa wanatakiwa kuhakikisha magari ya mizigo,mazao hayapakii abiria na atakaye kiuka agizo hili hatafikishwa mahakamani mala moja 
ambapo

Share: