BEST WISHES NELSON MANDELA

Ikiwa bado hali yake kiafya haijakaa sawa,Raisi wa zamani na mpigania uhuru wa afrika kusini Mh Nelson Mandela leo ametimiza miaka 95 tangu alipozaliwa tarehe kama ya leo mwaka huo.

Ikiwa kama uongozi wa blog hii inatoa pongezi kwa Nelson Mandela na familia yake kwa ujumla huku tukimtakia afya njema na apate nafuu haraka iwezekanavyo.


Hii hapa historia fupi ya Mandela
Nelson Rolihlahla Mandela alizaliwa tarehe 18 Julai, mwaka 1918. Ni rais wa kwanza aliyechaguliwa kidemokrasia nchini Afrika Kusini. Alikuwa mwanasheria na mwanachama wa ANC aliyepinga siasa ya ubaguzi wa rangi Apartheid katika Afrika Kusini. Mandela alitumikia kifungo cha maisha kwa miaka 27 kutokana na harakati zake za kuupinga ubaguzi wa rangi. Alifungwa katika kisiwa cha Robben. Baada ya kuachiliwa huru mwaka 1990 alianzisha sera ya maridhiano. Mwaka wa 1993, pamoja na Frederik Willem de Klerk alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Amani

HAPPY BIRTHDAY NELSON MANDELA



Share: