UHUSIANO WA SIKU SABA ZA WIKI NA KUZALIWA KWA MTOTO.

Katika wiki zipo siku saba na kila siku ipo sayari na jini na mafusho yanayosimamia siku hiyo.Mada yetu ya leo ni kuchambua mtoto akizaliwa katika siku hizi basi nguvu za kinyota zinamfanya awe vipi.



1. JUMATATU
Mtoto akizaliwa siku ya jumatatu atakuwa mtoto mpenda haki,mwenye sura nzuri,mwenye roho nzuri na msaada kwa watu.

2.JUMANNE
Mtoto akizaliwa siku ya jumanne atakuwa mtoto mwenye vipaji vingi na mzuri ambaye utaridhika kukaa naye, na mtu wa kupenda raha sana.

3.JUMA TANO
Mtoto akizaliwa siku ya jumatano atakuwa mtoto ambaye hatakuwa akicheka ovyo ovyo,atakuwa mtu serious na mchekeshaji,atakuwa mtu mwenye majonzi kila mara na atataka kubadili kila kitu.

4. ALHAMISI
Mtoto akizaliwa siku ya alhamisi atakuwa mtoto ambaye atakae fika mbali kimaisha,atakuwa mbunifu wa mambo,mfumbuzi wa mambo mengi sana na atategemewa sana na jamii.

5.IJUMAA
Mtoto akizaliwa siku ya ijumaa atakuwa mtoto mwenye kupendwa na watu,mtu wa kutegewa na watu na atapendwa sana na jamii.

6.JUMAMOSI
Mtoto akizaliwa siku ya jumamosi atakuwa akifanya kazi kwa bidii ili kumudu hali ya kimaisha,atakuwa ni mtu mwenye tamaa ya makuu,atakuwa mwenye kufanya kazi na kumaliza na atakuwa wakujua anachohitaji maishani.

7.JUMA PILI
Mtoto akizaliwa siku ya jumapili atakuwa ni mtoto mwenye busara,mpenda haki,mwenye hekima katika utu uzima wake,ni mwenye mapenzi ya kweli kwa watu wake na waliokaribu na yeye na atakuwa mwenye kuwaletea furaha kwa watakao kuwa wanaishi na yeye.

Chanzo-Sheikh Tariq Abdulaziz Mohamed
Share: