ANGALIA SHULE INAYOJENGWA JUU YA MAJI

Watoto katika wilaya ya Makoko laazima wajifunze kuogelea ikiwa wanataka kwenda shuleni. Kwa sababu wilaya hiyo katikati mwa mji mkuu wa Nigeria Lagos imekumbwa na mafuriko tangu mwezi Machi 2013. Shule inayoelea ni mfano wa usanifu majengo wa kiafrika "Afritecture". Usanifu huu unaweka kando dhana za ujenzi wa kimagharibi na kutegemea zaidi mbinu za kienyeji na vifaa kama vile mbao.


Share: