Malalamiko hayo ya wakulima yamekuja kufuatia tukio la ngombe 
za wafugaji kuuawa ambapo wakulima hao wametupia lawama jeshi la polisi 
kushindwa kuondoa mifugo katika maeneo ya wakulima kama ilivyoagizwa na serikali 
ya wilaya na kuwatuhumu askari kutumia nguvu kutawanya maandamano na baadhi ya 
wakulima kushikiliwa na jeshi la polisi.
Akizungumzia tuhuma hizo mkuu wa kituo cha polisi Turia Rajab 
Shemndolwa amesema wamelazimika kutumia nguvu kutokana na wananchi kutofuata 
taratibu za kufanya maandano na kukaidi amri ya jeshi na kwa kufunga barabara 
kwa mawe kwa zaidi ya masaa manne na kuzuia shughuli za usafiri.
Nae mkuu wa wilaya ya Mvomero Antony Mtaka akizungumzia tuki 
hilo amekiri uharibifu mkubwa uliofanywa baada ya mahindi kuliwa na mifugo  hali 
inayosababisha njaa kwa wakulima waliolima lakini kuwa mkakati wa serikali sasa 
ni kusikiliza malamiko ya pande zote mbili katika kutatua mgogoro huo.